Saturday, 13 April 2013

Mh MWIGULU KUIKWAZA MAHAKAMA? ADAI 'CHADEMA ILIPANGA KUTEKA NA KUUA'

mwigulu nchemba bungeni
Naibu katibu mkuu wa CCM ambaye pia ni mbunge wa Iramba Magharibi, Mh Mwigulu uenda akawa ametoa hukumu ya kesi ya ugaidi  kwa kudai kwamba 'CHADEMA walipanga kuteka na kuua'

Pamoja na kauli hiyo, akiogea kwa ghadabu kwenye kikao cha bunge, Mh Mwigulu alisema anao ushaidi wa kutosha na yupo tayari kutoa ushahidi mahakamani, polisi na hata mbinguni!

Huku akionyesha ushaidi wa karatasi lililo nakiliwa mikakati ugaidi iliyoelekezwa wakati wa mazungumzo, Mh Mwigulu alisema aliyeandika ni mwenye nyumba ambapo mazungumzo hayo yalifanyika ambaye naye yupo tayari kutoa ushahidi pamoja na aliyerekodi video ya ugaidi.

Mara nyingi swala likiwa mahakamani sio kawaida kutoa kauli kama hizi, labda hii ni tofauti!

Kuelewa zaidi twanga link:  http://www.youtube.com/watch?v=HIdFJn228Yo

No comments:

Post a Comment